Zawadi Tano za Ukarimu
- Dalvin Mwamakula
- Jan 9
- 2 min read

Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni. (Warumi 12:13)
Je! tunapata thawabu gani ikiwa tunaamini ahadi za Mungu, kutoa kwa moyo mkunjufu, na kufungua nyumba zetu kwa kila mmoja wetu na wahitaji?
Mateso ya watakatifu yataondolewa au angalau kupungua. Hiyo ndiyo maana ya mstari huu unaposema, “Changieni mahitaji ya watakatifu.” Tunainua mzigo. Tunaondoa msongo. Tunatoa matumaini. Na hiyo ni thawabu!
Utukufu wa Mungu unaonyeshwa. “Acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu, wapate kuona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni” (Mathayo 5:16). Utoaji wa kifahari na nyumba zilizo wazi huonyesha utukufu na wema na thamani ya Mungu katika maisha yako. Sababu ya Mungu kutupa pesa na nyumba ni ili kwa jinsi tunavyozitumia watu waone wao sio Mungu wetu. Lakini Mungu ni Mungu wetu. Na hazina yetu.
Shukrani zaidi kwa Mungu zinafunguliwa. “Huduma ya utumishi huu si tu kwamba inawatimizia watakatifu mahitaji yao, bali pia inazidi sana katika kutoa shukrani nyingi kwa Mungu” (2 Wakorintho 9:12). Mungu ametupa pesa na nyumba sio tu kutufanya tuwe na shukrani, bali kwa ukarimu wetu kuwafanya watu wengi kumshukuru Mungu.
Upendo wetu kwa Mungu na upendo wake ndani yetu umethibitishwa. “Ikiwa mtu yeyote ana mali ya dunia na akamwona ndugu yake ana uhitaji, lakini akamfungia moyo wake, upendo wa Mungu unakaaje ndani yake?” (1 Yohana 3:17). Kwa maneno mengine, tunapotoa kwa ukarimu na kufungua nyumba zetu, upendo wa Mungu unathibitishwa katika maisha yetu. Sisi ni halisi. Sisi si Wakristo wadanganyifu.
Hatimaye, tunaweka hazina mbinguni. “Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jipatieni mifuko isiyochakaa, na hazina isiyoisha mbinguni. . . . Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwa na moyo wako” (Luka 12:33–34).
Utoaji wa kifahari ni msingi wa maisha ya Kikristo, thawabu yetu ni utukufu wa Mungu na furaha ya kumthamini Kristo milele.
Utoaji wa kifahari na nyumba zilizo wazi ziko karibu na kitovu cha maisha katika Kristo. Sababu za kutofungua mifuko yetu ya pesa — vitabu vyetu vya hundi — na nyumba mara nyingi kama tunavyopaswa zinatokana na utumwa wa woga na uchoyo. Dawa ni furaha ya uwepo wa Kristo na uhakika wa ahadi ya Kristo: “Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu” (Wafilipi 4:19).
Thawabu yetu ni onyesho la utukufu wa Mungu, wema wa wengine, na furaha ya kumthamini Kristo pamoja milele. Kwa hiyo nawasihi, “Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni."




Comments