top of page

Habari Njema: Mungu Ana Furaha

  • Writer: Dalvin Mwamakula
    Dalvin Mwamakula
  • Jun 30
  • 2 min read
ree

“. . . Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa . . “. (1 Timotheo 1:11)


Hili ni tamko zuri sana katika kitabu cha 1 Timotheo, lililojificha chini ya uso wa kawaida wa maneno yanayojulikana sana katika Biblia. Lakini ukilichimbua vizuri, linasikika hivi: “habari njema ya utukufu wa Mungu mwenye furaha.” Neno “heri” katika kifungu hiki halimaanishi “asifiwe,” bali lina maana ya “mwenye furaha.”

 

Sehemu kubwa ya utukufu wa Mungu ni furaha yake.

 

Ilikuwa ni jambo lisilowezekana kwa mtume Paulo kufikiria kwamba Mungu angeweza kunyimwa furaha isiyo na mipaka na bado awe mwenye utukufu kamili. Kuwa na utukufu usio na mipaka kulimaanisha kuwa na furaha isiyo na mipaka. Alitumia msemo huu, “utukufu wa Mungu mwenye furaha,” kwa sababu ni jambo la utukufu kwa Mungu kuwa na furaha jinsi alivyo.

 

Utukufu wa Mungu kwa sehemu kubwa upo katika ukweli kwamba Yeye ana furaha kuliko tunavyoweza kufikiria. Kama mhubiri mkuu wa karne ya kumi na nane, Jonathan Edwards, alivyosema, “Sehemu ya ukamilifu wa Mungu anaoshirikisha ni furaha yake. Furaha hii ipo katika kujifurahia na kujishangilia mwenyewe; na vivyo hivyo ndivyo furaha ya viumbe wake inavyopatikana.”

 

Na hili ni sehemu muhimu ya injili, Paulo anasema: “injili ya utukufu wa Mungu mwenye furaha.” Ni habari njema kwamba Mungu ana furaha yenye utukufu. Hakuna mtu ambaye angependa kukaa milele na Mungu mwenye huzuni na asiye na furaha.

 

Ikiwa Mungu hana furaha, basi lengo la injili kukaa na Mungu milele si lengo lenye furaha, na hivyo injili hiyo isingekuwa injili hata kidogo.

Lakini, kwa kweli, Yesu anatualika tukae milele na Mungu mwenye furaha anaposema, “Ingia katika furaha ya bwana wako” (Mathayo 25:23).

 

Yesu alisema katika Yohana 15:11, “Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu iwe timilifu.” Yesu alizungumza, akaishi, na akafa ili furaha yake—furaha ya Mungu—iwe ndani yetu na furaha yetu iwe kamili. Hivyo basi, injili ni “injili ya utukufu wa Mungu mwenye furaha.”

Comments


100Fold Logo

NJIA ZA KUTUFUATILIA

  • Youtube
  • WhatsApp
  • Email
  • Facebook
  • Instagram
bottom of page