Huwezi kushindwa Mwishoni
- Dalvin Mwamakula
- Mar 31
- 2 min read

“Ninyi mnao askari walinzi. Nendeni, liwekeni ulinzi kadri mwezavyo.” (Mathayo 27:65)
Yesu alipokuwa amekufa na kuzikwa, huku jiwe kubwa likiwa limeviringishwa kwenye kaburi, Mafarisayo walimwendea Pilato na kumuomba ruhusa ya kulifunga jiwe hilo na kulilinda kaburi.
Walijaribu kwa bidii yao yote — bila mafanikio.
Kulikuwa hakuna matumaini wakati huo, hakuna matumaini leo, na itakuwa bila matumaini daima. Wajaribu wawezavyo, watu hawawezi kumzuia Yesu. Hawawezi kumshikilia kaburini.
Si vigumu kuelewa: Anaweza kutoroka kwa sababu hakulazimishwa kuingia. Alijiruhusu kukashifiwa na kunyanyaswa, kuteswa, kutengwa na kudharauliwa na kusukumwa huku na kule na kuuawa.
Nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna anayeuchukua, bali mimi nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninayo mamlaka ya kuutoa, na ninayo mamlaka ya kuutwaa tena. (Yohana 10:17-18)
Hakuna anayeweza kumuweka chini kwa sababu hakuna aliyewahi kumwangusha. Aliutoa alipokuwa tayari.
Wakati inaonekana kama amezikwa kabisa, Yesu anafanya kitu cha kushangaza kwenye giza. “Ufalme wa Mungu ni kama mtu atawanye mbegu juu ya ardhi. Yeye hulala na kuamka usiku na mchana, na mbegu huota na kukua; pasipo yeye kujua ikuavyo ” (Marko 4:26–27).
Dunia inadhani Yesu ameshindwa mazima — hayupo tena — lakini Yesu anafanya kazi katika sehemu za giza. “mbegu ya ngano isipoanguka katika ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake; lakini ikifa, huzaa matunda mengi” (Yohana 12:24). Aliruhusu azikwe - "hakuna mtu anayeniondoa [maisha yangu]" - na atatoka kwa mamlaka wakati na mahali anapopenda - "Nina mamlaka ya kuuchukua tena."
"Mungu alimfufua, kutoka kwa wafu akimwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti" (Matendo 2:24). Yesu ana ukuhani wake leo "kwa uwezo wa uzima usioharibika" (Waebrania 7:16).
Kwa karne ishirini, dunia imejaribu kwa bidii yao yote — bila mafanikio. Hawawezi kumzika. Hawawezi kumshikilia ndani. Hawawezi kumnyamazisha au kumwekea mipaka. Yesu yuko hai na ana uhuru kamili wa kwenda na kuja popote anapotaka.
Muamini na uende naye, haijalishi nini kitatokea. Huwezi kushindwa mwishowe.
Comments