Neema ya Mungu katika Karama za Kiroho
- Dalvin Mwamakula
- Jun 30
- 2 min read

Kila mmoja na atumie kipawa chochote alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu. (1 Petro 4:10)
Tunapotumia vipawa vyetu vya kiroho, sisi ni wasimamizi wa neema - sio neema ya jana, lakini ya leo, inayofika katika kila wakati wa uhitaji. Na neema hii ya wakati ujao ni “neema tofauti tofauti. Inakuja kwa rangi nyingi na maumbo mengi na saizi tofauti. Hii ni sababu mojawapo ya karama za kiroho katika mwili kuwa tofauti sana. Mtazamo wa kipekee wa karama za Mungu katika maisha yako utaangaza utukufu wa Mungu kwa namna ambayo usingeweza kuonekana kupitia maisha yangu.
Kuna neema nyingi za wakati ujao kama kulivyo na mahitaji katika mwili wa Kristo - na zaidi.
Kusudi la karama za kiroho ni kupokea na kusambaza neema ya Mungu ya wakati ujao kwa mahitaji hayo.
Lakini mtu anaweza kuuliza, “Kwa nini mnamchukua Petro kurejea neema ya wakati ujao? Je, msimamizi si msimamizi wa duka la familia ambalo tayari lipo?”
Sababu kuu ya kuchukua Petro kurejelea neema ya baadaye ni kwa sababu mstari unaofuata unaonyesha jinsi hii inavyofanya kazi, na marejeleo hapo ni kwa usambazaji unaoendelea wa neema ya wakati ujao. Anasema, “Yeyote anaye hudumu, [na haudumu] kwa nguvu zinazotolewa na Mungu —ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kupitia Yesu Kristo” (1 Petro 4:11). Neno ni “inayotolewa,” sio “iliyotolewa.” Unapohudumu, hudumu kwa uwezo wa ugavi unaoendelea wa neema ya Mungu kufanya kile unachohitaji kufanya.
Unapotimiza karama yako ya kiroho ya kuhudumumia mtu kesho, utakuwa unakuwa ukihududumu “kwa nguvu ambazo Mungu hutoa” - na ugavi utakuwa kesho, sio leo. “Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako” (Kumbukumbu la Torati 33:25).
Mungu anaendelea, siku baada ya siku, muda baada ya muda, akitoa “nguvu” tunapohudumu. Anafanya hivyo kwa sababu msambazaji anayeendelea, asiye na mwisho wa nguvu anapata utukufu. “Yeyote anayehudumu, [na ahudumu] kwa nguvu anazojaliwa na Mungu—ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kupitia Yesu Kristo.”




Comments