top of page

Rehema kwa ajili ya Leo

  • Writer: Dalvin Mwamakula
    Dalvin Mwamakula
  • Mar 31
  • 1 min read

Upendo thabiti wa Bwana haukomi; fadhili zake hazikomi kamwe; ni mpya kila asubuhi; uaminifu wako ni mkuu. (Maombolezo 3:22–23)

 

Rehema za Mungu ni mpya kila siku asubuhi kwa sababu kila siku ina rehema ya kutosha ndani yake kwa siku hiyo. Mungu anapanga matatizo ya kila siku. Na Mungu huweka rehema za kila siku. Katika maisha ya watoto wake, yamepangwa kikamilifu. Yesu alisema, “Kwa hiyo msiwe na msisumbukie juu ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku taabu yake yenyewe” (Mathayo 6:34). Kila siku ina shida yake. Kila siku ina rehema zake. Kila asubuhi ni mpya.


Lakini mara nyingi tunakata tamaa tunapofikiria kwamba huenda tukalazimika kubeba mzigo wa kesho kwa rasilimali za leo. Mungu anataka tujue: Hatutalazimika kufanya hivyo.


Rehema za leo ni za shida za leo. Rehema za kesho ni za shida za kesho.

Wakati mwigine tunajiuliza kama tutakuwa na rehema ya kusimama katika majaribu ya kutisha. Ndiyo, tutafanya hivyo. Petro anasema, “Mkitukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa utukufu na wa Mungu anakaa juu yenu” (1 Petro 4:14). Wakati matukano yanapokuja, Roho wa utukufu huja. Ilitokea kwa Stefano alipokuwa akipigwa mawe. Itatokea kwako pia. Wakati Roho na utukufu vinahitajika, vitakuja.


Mana kule jangwani ilitolewa siku moja baada ya nyingine. Hakukuwa na kuhifadhi. Ndivyo tunavyopaswa kutegemea rehema za Mungu. Hupokei leo nguvu ya kubeba mizigo ya kesho. Unapewa rehema leo kwa shida za leo.


Kesho rehema zitakuwa mpya. “Mungu ni mwaminifu, ambaye mliitwa katika ushirika wa Mwana wake Yesu Kristo Bwana wetu” (1 Wakorintho 1:9).

Comments


100Fold Logo

NJIA ZA KUTUFUATILIA

  • Youtube
  • WhatsApp
  • Email
  • Facebook
  • Instagram
bottom of page