Ufunguo wa Upendo Thabiti
- Dalvin Mwamakula
- Mar 31
- 2 min read

“Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo kwa ajili yangu. Furahini na kushangilia, kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.” (Mathayo 5:11-12)
Mojawapo ya maswali niliyouliza nilipokuwa nikihubiri juu ya kuwapenda adui zetu kutoka katika Mathayo 5:44 lilikuwa, Je, unawapendaje watu wanaokuteka nyara na kukuua?
Tunawezaje kufanya hivyo? Nguvu ya kupenda namna hii inatoka wapi? Hebu fikiria jinsi hii inavyoshangaza inapoonekana katika maisha halisi! Je, kuna chochote kinachoweza kuonyesha ukweli na nguvu na uhalisi wa Kristo zaidi ya hili?
Ninaamini kwamba Yesu anatupa ufunguo wa upendo wa msimamo huu na wa kujidhabihu, uliofafanuliwa katika Mathayo 5:44, hapo awali katika sura iyo hiyo.
Katika Mathayo 5:11-12, anazungumza tena juu ya kuteswa, kama vile alivyokuwa wakati aliposema katika Mathayo 5:44, "Wapendeni adui zenu na waombeeni wanaowaudhi." Kinachohajabisha kuhusu mistari hii ni kwamba Yesu anasema kwamba haitoshi kustahimili mateso ya adui pekee, bali furahia ndani yoa. “Umebarikiwa wewe wengine wakikutukana na kukutesa. . . . Furahini na kushangilia.”
Hili linaonekana kuwa nje ya uwezo wetu kuliko kuombea adui zetu au kuwatendea mema. Ikiwa ningeweza kufanya jambo hili lisilowezekana kibinadamu - yaani, kufurahia kuteswa - basi ingewezekana kuwapenda watesi wangu. Ikiwa muujiza wa furaha katikati ya hofu ya udhalimu na maumivu na kupoteza inaweza kutokea, basi muujiza wa upendo kwa wahalifu unaweza kutokea pia.
Yesu anatupa ufunguo wa furaha katika mistari hii. Anasema, “Furahini na kushangilia, kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni.” Ufunguo wa furaha ni imani katika neema ya Mungu ya wakati ujao - yaani, kuridhika katika yote ambayo Mungu anaahidi kuwa kwako. Anasema, “Furahini, kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni.” Furaha yetu katika mateso ni furaha ya mbinguni inayorudi katika wakati huu wa hofu na kutuweka huru kupenda. Kwa hiyo, furaha hii ndiyo nguvu inayoweka huru ya kuwapenda adui zetu wanapotutesa.
Ikiwa hiyo ni kweli, basi amri ya kupenda kwa uwazi pia ni amri ya kukazia mawazo yetu juu ya mambo yaliyo juu - ambayo Mungu anaahidi kuyafanya yetu - sio juu ya vitu vilivyo duniani (Wakolosai 3: 2).
Amri ya kumpenda adui yetu ni amri ya kupata tumaini letu na uradhi wetu wa ndani kabisa wa nafsi kwa Mungu na thawabu yake kuu - neema yake ya wakati ujao. Ufunguo wa upendo thabiti ni imani katika neema ya baadaye. Ni lazima tushawishike katikati ya uchungu wetu kwamba upendo wa Mungu ni "bora kuliko uhai" (Zaburi 63:3).
Kumpenda adui yako haikupatii thawabu ya mbinguni. Kuithamini thawabu ya mbinguni kunakupa uwezo wa kumpenda adui yako.
Commentaires