Upole Ni Nini?
- Dalvin Mwamakula
- Apr 28
- 2 min read
Updated: May 1

“Heri walio wapole, maana hao watairithi nchi.” (Mathayo 5:5)
Upole huanza tunapoweka tumaini letu kwa Mungu. Kisha, kwa sababu tunamwamini, tunaweka njia zetu kwake. Tunaweka kwake mahangaiko yetu, fadhaa zetu, mipango yetu, mahusiano yetu, kazi zetu, afya zetu.
Na kisha tunamngojea Bwana kwa saburi.
Tunaamini katika wakati wake na nguvu zake na neema yake kufanya mambo kwa njia bora zaidi kwa utukufu wake na kwa manufaa yetu.
Matokeo ya kumwamini Mungu, na kutwika mahangaiko yetu kwa Mungu, na kumngojea kwa subira ni kwamba hatutoi nafasi ya kuwa na wasiwasi na hasira kwa haraka. Lakini badala yake, tunatoa nafasi kwa ghadhabu na kukabidhi suala letu kwa Mungu na kumwacha atutetee apendavyo.
Na kisha, kama Yakobo asemavyo, katika ujasiri huu tulivu sisi tusiwe wepesi wa kusema na wepesi wa kusikiliza (Yakobo 1:19). Tunakuwa wenye busara na tayari kusahihishwa (Yakobo 3:17). Yakobo anauita huu “upole wa hekima” (Yakobo 3:13).
Upole hupenda kujifunza. Na inahesabu mapigo ya kurekebishwa na rafiki kuwa ya thamani (Mithali 27:6). Na inapobidi iseme neno la kukosoa kwa mtu aliyenaswa katika dhambi au makosa, inazungumza kutokana ushawishi wa kina wa makosa yake mwenyewe na uwezekano wake wa kutenda dhambi na utegemezi wake kamili juu ya neema ya Mungu (Wagalatia 6:1).
Utulivu na uwazi na kuwa tayari kupatwa na lotote kwa upole ni kuzuri sana na kunaumiza sana. Inakwenda kinyume na yote tulivyo kwa asili yetu ya dhambi. Inahitaji msaada wa kiungu.
Ikiwa wewe ni mfuasi wa Yesu Kristo - ikiwa unamwamini na kuweka njia yako kwake na kumngojea kwa subira - Mungu tayari ameanza kukusaidia na atakusaidia hata zaidi.
Na njia ya msingi ambayo atakusaidia ni kuuhakikishia moyo wako kwamba wewe ni mrithi mwenza wa Yesu Kristo na kwamba ulimwengu na vyote vilivyomo ni vyako (1 Wakorintho 3:21–23). Wenye upole watairithi nchi.




Comments