top of page

Athari za Maisha Yako Baada ya Miaka 1,400

  • Writer: Dalvin Mwamakula
    Dalvin Mwamakula
  • Apr 3
  • 3 min read

Makala imeandwika na John Piper

Mwanzilishi na Mwalimu, desiringGod.org


Je, unafikiri Mungu ana makusudi kwa ajili ya maisha yako ambayo yatatimizwa baada ya miaka 1,400? Mimi nafikiri hivyo. Maisha yako na yangu.


Ndiyo, mbingu mpya na nchi mpya zinaweza kuwapo kufikia wakati huo. Natumaini hivyo. Ikiwa ndivyo, kuna mambo ambayo yanatokea kwako sasa ambayo yatakuwa na athari fulani wakati huo kwa faida yako.


Ninasema hivyo kwa sababu Paulo anasema, “Mateso haya mepesi ya kitambo yanatuandalia uzito wa milele wa utukufu usio na kifani” ( 2 Wakorintho 4:17). Paulo anapozungumza kuhusu “dhiki nyepesi ya kitambo,” anarejelea uzoefu wote wenye uchungu wa maisha yetu — kitu kile kile anacho maanisha kwa “mateso ya wakati huu wa sasa” katika Warumi 8:18. Wakati huu wote wa sasa.


Katika utawala wa Mungu wa ulimwengu, kila kitu kinahusiana na kila kitu.

Na anaposema kwamba matukio haya ya maisha marefu “yanatuandalia uzito wa milele wa utukufu,” anamaanisha kwamba kuna uhusiano kati ya matukio hayo sasa na uzoefu wetu wa utukufu baadaye. Na uwiano huo ni zaidi ya mfuatano, na zaidi ya ushahidi kwamba tunaenda kwenye utukufu.


Isingemfariji sana Paulo ikiwa ningelisema kwamba hoja kuu ni: “Jinsi ninavyoshughulikia maumivu ya mgongo wangu na jinsi unavyoshughulikia kukatwa kichwa kwako ni uthibitisho wa kwamba sote tutapata utukufu.” Hiyo ni kweli. Lakini sio maana ya neno "kutayarisha"(katergazetai). Kukatwa kichwa kwake kutakuwa na athari tofauti kwa utukufu wake kuliko maumivu yangu ya mgongo juu yangu. Nami nitafurahi zaidi kwa thawabu yake.


Kila Kitu Kinahusiana na Kila Kitu

Lakini vipi ikiwa, ndani ya miaka 1,400 Kristo atakuwa bado hajarudi? Je, maisha yako yataleta mabadiliko katika ulimwengu huo? Nafikiri hivyo. Katika utawala wa Mungu wa ulimwengu, kila kitu kinahusiana na kila kitu.


Chunguza mfano huu.

Wakati nilipokuwa Ethiopia mwezi Novemba mwaka jana, niliambiwa kuhusu mmisionari Mwethiopia aliyekwenda Pakistani. Aliingia katika mji kwa nia ya kutaka kufanya uinjilisti na kuanzisha kanisa, ingawa Pakistani haiko wazi kwa aina hii ya kazi ya umisionari.


Lakini alipokwenda mbele ya viongozi wa mji na wakagundua kwamba alitoka Ethiopia walisema hivi: “Mnaweza kufanya kazi yenu hapa. Tuna deni kwako zawadi ya uwazi na ukarimu, kwa sababu watu wako walitoa hifadhi kwa familia ya Muhamad miaka 1,400 iliyopita.”


Haki ya Ardhi

Tangu wakati huo nimejaribu kufuatilia historia nyuma ya kauli hii ya kushangaza. Mnamo 2008 kulikuwa na kongamano kuhusu mila hii. Wasomi kutoka Princeton, Cornell, Rutgers, na Jumba la Makumbusho la Kitaifa la Ethiopia walikutana ili kujadili matokeo mapya ya kihistoria.


Katika historia na mapokeo ya Kiislamu, Ethiopia (Abyssinia) inajulikana kama “Kimbilio la Hijra ya Kwanza” ya Waislamu. Wakati wa uhai wa Muhamad (570 – 632) wafuasi wake walikuwa wakiteswa katika mazingira ya Makka na makabila ya kipagani.


Chochote Kile tunachofanya kwa kumtii Kristo katika maisha haya hakipotei bure.

Dk. Said Samatar, Profesa wa Historia ya Kiafrika huko Rutgers, alielezea "Mfalme Armah (Negash) na uamuzi wake wa kutoa hifadhi kwa familia ya Mtume Mohammad, ambaye alifika Aksum wakati akiwakimbia watesi wao wapagani." Mfalme Armah alikuwa Mkristo na alikuwa na sifa ya kuwatendea watu kwa ukarimu. Dakt. Samatar alieleza jinsi “Mfalme Mkristo alikataa rushwa na kuwapa hifadhi Waislamu waliokimbia huko Aksum.”


"Mohammad hakusahau ukarimu wa Wanegash," alisema, "na katika maneno (hadith) ya Mtume ambayo yameandikwa na kupitishwa kwa vizazi kadhaa, imebainishwa kwamba 'Abyssinia [Ethiopia] ni nchi ya haki ambayo hakuna mtu anayedhulumiwa.'


Kwa hivyo, kwa Waislamu wengi hata leo, miaka 1,400 baadaye, "Ethiopia ni sawa na uhuru kutoka kwa mateso na kukombolewa kutoka kwa woga."


Zingatia Athari Yako

Je, unafikiri kwamba Wakristo wa Abysinnia, miaka 1,400 iliyopita walifikiri kwamba walichokuwa wakifanya kingekuwa na matokeo kwa ajili ya utukufu wa Kristo na wema wa ulimwengu karne kumi na nne baadaye, wakati meya wa Pakistani alipofungua jiji lake kwa mmisionari Mkristo kutoka Ethiopia?


Kwa hiyo, ninahitimisha kwamba kile tunachofanya kwa kumtii Kristo katika maisha haya hakipotei bure. Matendo yetu ni kama kokoto zilizodondoshwa kwenye bwawa la historia. Haijalishi kokoto yetu ni ndogo kiasi gani, Mungu hutawala mawimbi. Na anaufanya mpango juu ya uso wa maji kuwa vile apendavyo. Kokoto zako zinahesabiwa, na zina thamani. Zidondoshe kwa uaminifu wa kila siku, na yaachie mawimbi kwa Mungu.

 

Comments


100Fold Logo

NJIA ZA KUTUFUATILIA

  • Youtube
  • WhatsApp
  • Email
  • Facebook
  • Instagram
bottom of page