top of page
Painted Space
Furaha Thabiti Cover page_edited_edited_
20.png


"Maneno yako ni matamu kama nini kwangu, Ni matamu kuliko asali kinywani mwangu!"

 

23.png


"Furaha ya Mungu katika Mwana wake itakuwa ndani yetu na itakuwa yetu - furaha yetu katika Mwana. Na hili halitaisha, kwa sababu Baba wala Mwana hawana mwisho."
 

26.png

"Mungu anapenda kuonyesha uungu wake kwa kunifanyia kazi, na kazi yake kwangu daima ni kabla na chini, ndani, na katika kazi yoyote ninayofanya kwa ajili yake."
 

29.png


"Mwili wa nani? wa Kristo. Dhambi ya nani ilihukumiwa katika mwili huo? Zetu. Kwetu sisi basi? Hakuna hukumu! "
 

32.png


"Kwasababu kiini cha utukufu wake ni utimilifu wa neema inayofurika katika wema kwa wahitaji."
 

35.png

"Wivu wa Mungu ni tishio kwa wanaofanya ukahaba na kuiuza mioyo yao kwa ulimwengu, lakini ni faraja kwa wanaoshika nadhiri za agano na kuwa wageni duniani."

38.png

"Ubinafsi unatafuta furaha ya kibinafsi kwa gharama ya wengine.  Upendo kama wa Kristo unatafuta furaha yake katika furaha ya wengine - si kwa gharama zao."

41.png

"Wake, tafuteni furaha yenu kwa kuthibitisha na kuwaheshimu waume zenu kama viongozi. Waume, tafuteni furaha yenu kwa kuwaongoza na kujitoa kwa wake zenu kama Kristo alivyofanya kwa kanisa."

44.png


"Neema kuu ya Mungu, inayofanya yasiyowezekana kwa wanadamu, kupitia injili ya Yesu Kristo, ndiyo tumaini kuu la kimishonari."
 

47.png


"Kwa wamisionari watarajiwa, Yesu anasema, “Naahidi kufanya kazi kwa ajili yenu, na kuwa kwa ajili yenu, kiasi kwamba hamtaweza kusema kuwa mmetoa dhabihu yoyote.”"

50.png


"Kila hatua muhimu niliyowahi kuchukua katika kuelewa kina cha upendo wa Mungu na kukua kwa undani naye imekuja kupitia mateso."

 

20.png


"Mungu hatosheki kamwe kutupa ulinzi wa moto wake; analenga kutupa raha ya uwepo wake. Ninazipenda "Nita" za Mungu!"


 

23.png


"Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, dhiki, au shida, au mateso, au njaa, au utupu, au hatari, au upanga?"


 

26.png


"Je, si upumbavu kukubali mkataba wa neema kisha kupanga njia ya kuilipia? Neema inapaswa kuwa bure, hivyo hatuwezi kuichukulia kama kitu kinachohitaji kulipiwa."
 

29.png


"Wasiwasi haufanyi chochote cha maana. Hiyo ni ahadi. Iamini. Itendee kazi."

32.png


"Furaha ya kuwa na Yesu ni mstari usiokatika kutoka sasa hadi umilele. Hautokatwa - si kwa kifo chake au chetu."
 

35.png


"Ili tuwe huru kabisa, ni lazima tuwe na shauku, uwezo, na fursa ya kufanya mambo ambayo yatatufanya tuwe na furaha milele. Bila majuto."
 

38.png


"Msijisumbue juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu zijulikane na Mungu."

41.png


"Kazi kubwa ya upendo ilifanikishwa kwa sababu Yesu alitafuta furaha kuu zaidi: kutukuzwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu katika kusanyiko la waliokombolewa."

44.png


"Ahadi za neema ya Mungu zinatoa nguvu zinazofanya matakwa ya utakatifu wa Mungu kuwa uzoefu wa uhuru badala ya hofu na kifungo."
 

47.png


"Sifa ya kweli inamaanisha furaha kamili, na kusudi la juu kabisa la mwanadamu ni kunywa kwa kina katika furaha hii kwa ajili ya utukufu wa Mungu."

16.png

Kwanini Una Mwili


Ndiyo maana unao mwili sasa. Na ndiyo maana utafufuliwa kuwa kama mwili wa utukufu wa Kristo.
 

19.png

Yesu Alinunua Uvumilivu Wako

Baba ndiye aliyepanga. Yesu aliinunua. Roho Mtakatifu anatekeleza kivitendo — Wote pasipo kushindwa. 

22.png

Mwisho wa Injili

Wema wa juu zaidi, kamili, wa ndani, mtamu zaidi wa injili ni Mungu mwenyewe, anayefurahiwa na watu wake waliokombolewa.
 

25.png

Nafsi Yangu Ina Kiu ya Mungu

Tunakuja kumpenda Mungu, na tunataka kumwona Mungu na kuwa na Mungu na kuridhika kwa kumtukuza na kumfurahia Mungu.

28.png

Kusudi La Kuumbwa Kwetu



Je, jibu la hakika ni, “Kwa sababu ninataka kumfurahia Mungu sasa na milele”?


 

31.png

Matumaini ya Kutii Amri Ngumu


Utafaidika zaidi kutii kila wakati kuliko kutomtii Yesu, hata ikiwa utii huo unagharimu maisha yako. 
 

34.png

Mungu Mwenye Furaha Isiyotikisika

Kwa hiyo, utafutaji wa Mungu wa sifa kutoka kwetu na utafutaji wetu wa furaha ndani yake ni utafutaji mmoja. 
 

37.png

Ujumbe wa Uumbaji:

Mchana na usiku vinasema jambo moja: Mungu ni mtukufu! Mungu ni mtukufu! Mungu ni mtukufu! Jiepushe na uumbaji kama furaha yako kuu, na umfurahie Bwana wa utukufu.

40.png

Yesu Atawakanyaga Maadui Zetu Wote

Kwa hiyo, kumbuka kwamba kiwango cha utawala wa Kristo kinamfikia kila adui mdogo na mkubwa wa utukufu wake katika maisha yako, na katika ulimwengu huu. Atashindwa.
 

43.png

Ukuaji wa Kanisa Kwa Njia ya Mungu


Kwa vyovyote vile, fanya kazi. Lakini daima mtazame Bwana kwa ajili ya kazi ya kimiujiza yenye maamuzi kamili. 

 

11.png

“Tuombe pamoja kwamba Mungu wetu mkuu asiye na mwisho aelekeze mioyo yetu kwake, na afungue macho yetu ili tumwone kadiri tuwezavyo, na tuwe na shauku ya kumjua zaidi.”

14-min.png


“Tunaweza kuwa na uhakika kwamba makosa yote yatashughulikiwa na Mungu na kwamba tunaweza kuyaacha mikononi mwake kwa sababu kisasi ni cha Bwana.”
 

17.png


“Imani inayookoa ni kutambua uchukizo wa dhambi, utakatifu wa Mungu, na uzuri wa msamaha wake, na kutamani urafiki mpya na Mungu mwenye kusamehe.”

 

20.png

“Kwa hiyo, Roho alikuja mara ya kwanza, na Roho anaendelea kusambazwa, kwa njia ya imani. Chochote anachofanya ndani na kupitia kwetu ni kwa imani.”
 

23.png

“Huduma ni mtindo wa maisha unaojitoa kwa Kristo na kukidhi mahitaji ya wengine, ikifanywa na Wakristo wa kawaida waliotayarishwa na Wachungaji wao.”

26.png

“Kuna neema ya ajabu 
Ya siku zijazo ya kutarajiwa 
wakati wa uhitaji. Kila tendo jipya la nguvu linashuhudia neema isiyobadilika inayotolewa kila wakati.”

29.png


“Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako.”

 

32.png

“Imani haitosheki na “anasa za haraka.” Ina njaa kubwa kwa ajili ya furaha. Furaha inayodumu. Milele.”
 

35-min.png

“Moyo unaopenda pesa—hutegemea pesa kwa ajili ya furaha—hautegemei utoshelevu wa Mungu ndani ya Yesu.”
 

38-min.png

“Kifo cha mashahidi sio jambo la bahati mbaya. Haikumshangaza Mungu. Si kitu kisichotarajiwa.”
 

8.png

Imani Inayokuza Neema

“Nilichofikiria ni, Ndiyo! Ninakuhitaji! Ninakushukuru! Napenda nguvu zako! Nimependa mpango wako! Ninapenda namna unavyonishikilia! Wewe ni mkuu!”

11.png

Kinachomfanya Mungu Ajivunie

“Kwa hiyo, fungua macho yako uione nchi iliyo bora zaidi, jiji la Mungu ambalo ametutayarishia, na ujiruhusu kulitamani kwa moyo wako wote. Mungu hataona haya kuitwa Mungu wako.”

14.png

Tunaishi kwa Imani


“Imani inayohalalisha na inayotakasa sio aina mbili tofauti. "Kutakasa" ni mchakato wa kubadilishwa kuwa kama Kristo, na yote yanatokana na neema.”
 

17.png

Wakati Akili Inapotumikia Uasi



“Mioyo yetu hutumia akili zetu kuhalalisha matamanio yetu, ili yaonekane sawa, hata kama sio.”
 

20.png

Nani Alimuua Yesu?

“Msingi wa ahadi ya neema ya Mungu ni kwamba Mwana wa Mungu alibeba adhabu yangu, ili niweze kusimama mbele ya Mungu nikiwa nimesamehewa na kufurahia ahadi za milele.”

23.png

Mtumikie Mungu kwa Kiu yako


“Je, unaihudumiaje chemchemi? 
Je, unahudumiaje  chombo cha umwagiliaji?
Je, unamtukuzaje Mungu 
kwa jinsi alivyo halisi?”

 

26.png

Kosa la Kuogopa Mwanadamu

“Unafikiri wewe ni nani kumwogopa mwanadamu na kunisahau mimi Muumba wako!”

29.png

Jinsi Tunavyopaswa Kupigania Utakatifu

“Kwa hiyo, kuna utakatifu ambao bila yake hakuna mtu atakayemwona Bwana. Na kujifunza kupigania utakatifu kwa imani katika neema ya wakati ujao ni muhimu sana. ”

32.png

Mtego wa Kifo Unaoitwa Tamaa

"Kilicho hatarini katika kukimbia tamaa na kupigania kuridhika kwa imani katika neema ya siku zijazo ni uzima wa milele."
 

35.png

Kuvumilia Wakati Kutii Kunaumiza


"Kwa maneno mengine, iweni imara sasa katika vyote mlivyopoteza kwa ajili ya Kristo, kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yenu."

 

6.png

VITAMBAA VICHAFU
HAKUNA TENA

"Watakatifu wa Agano la Kale walijua kwamba hivi ndivyo walivyookolewa, na kwamba imani hii ilikuwa ufunguo wa utii, na kwamba utii huo ulikuwa ushahidi wa imani hii."
 

9.png

Msukumo Hatarishi


"Imani inatazama ahadi, nitakuwa "pamoja nawe popote uendako", na kisha hujitokeza, kwa utii, kuichukua nchi."

 

12.png

Usimtumikie Mungu

"Lakini je, hakuna kitu tunachoweza kumpa Mungu ambacho hakitamshusha hadhi na kumfanya mfadhiliwa?

Kipo. Wasiwasi wetu. Mahitaji yetu. Vilio vyetu vya kuomba uwezo wa kufanya mapenzi yake."

15.png

Watu kwa ajili ya Jina Lake


"Haiwezekani kusisitiza zaidi umuhimu wa jina la Mungu, yaani, umaarufu wa Mungu, katika kuhamasisha utume wa kanisa."
 

18.png

Mwisho wa Yote

"Je, unaweka wazi kuwa uongofu wako umetokana na Mungu kikamilifu? Je, yeye ndiye kiini cha yote? Je, hii inakufanya uusifu utukufu wa neema yake kuu, inayoshinda?"

21.png

Upendo wa Bure


"Mungu ametuchagua sisi bure. Si kwa sababu ya kitu chochote ndani yetu, lakini kwa sababu Mungu alifurahia tu kufanya hivyo."

24.png

Kile Kinachomfanya Yesu Afurahi

"Yesu anafurahi katika Roho Mtakatifu na uchaguzi wa Baba yake anapowaokoa watu kwa neema yake ya bure."

27.png

Yesu Anawajua Kondoo Wake

"Kujulikana kibinafsi, kwa ukaribu, na kwa upendo na Mwana wa Mungu ni upendeleo mkubwa na zawadi ya thamani, ikijumuisha ushirika binafsi na ahadi ya uzima wa milele."

30.png

Makusudi ya Mungu Katika Njia Zisizonyooka


"Je, jambo lolote linalofanywa kwa jina la Kristo linaweza kupotea bure?"

33.png

Malipo ya Uvumilivu


"Hadithi ya Yusufu inatufundisha kuwa na imani katika neema ya Mungu kwa siku zijazo."

 

36.png

Faida ya Kumtumikia Mungu


"Imani haiwezi kujivunia wema, umahiri, au hekima ya kibinadamu kwani inategemea neema ya bure ya Mungu."
 

6.png

Jinsi ya Kujibu Unapokosea

"Hakuna unafiki. Hakuna kujifanya. Hakuna ukamilifu wa kujivunia. Hakuna tabasamu bandia au furaha ya juu juu."
 

9.png

Njia Mbili za Kumkumbuka Yesu

"Haijalishi ukali wa mateso, baya zaidi la kutokea duniani ni kifo, lakini Yesu ameondoa uchungu wa kifo. Yuko hai, nawe utakuwa hai."
 

12.png

Zungumza na Mungu, Sio tu Kumhusu 

"Somo tunaloweza kujifunza kutoka kwa muundo huu ni kwamba ni vizuri kutozungumza kwa muda mrefu juu ya Mungu bila kuzungumza na Mungu."

15.png

Huwezi kushindwa Mwishoni 


"Muamini na uende naye, haijalishi nini kitatokea. Huwezi kushindwa mwishowe."

18.png

Usiwe Kama Nyumbu

"Njia ya kuepuka kuwa kama nyumbu ni kujinyenyekeza, kuomba, kukiri dhambi, na kukubali mwongozo wa Mungu kwa ulinzi na riziki."

21.png

Mungu, Iguse Mioyo Yetu

"Ee Bwana, njoo. Njoo karibu zaidi. Njoo kwa moto, kwa maji, kwa upepo au tetemeko. Au njoo kwa utulivu na upole. Njoo mpaka utufikie sisi"

24.png

Ufunguo wa Upendo Thabiti

"Kumpenda adui yako haikupatii thawabu ya mbinguni. Kuithamini thawabu ya mbinguni kunakupa uwezo wa kumpenda adui yako."
 

27.png

Nguvu ya Ukombozi ya Msamaha

"Lazima tupambane na kutoamini na aibu inayolemaza kwa kushikilia ahadi za neema na amani zinazokuja kupitia msamaha wa matendo yetu."

30.png

Watoto wa Mungu Anayeimba



"Loo, siwezi kusubiri kumsikia Yesu akiimba!"
 

33.png

Mbinu Kumi na Tano za Furaha

"Katika maisha haya ya dhambi na maumivu, furaha inahitaji kupiganiwa kama imani. Paulo anatuambia, “Pigana vile vita vizuri vya imani."
 

4_edited.png

Mungu Hufanya Kazi Kupitia Maazimio Mema

"Mungu kamwe hataonekana kwa nguvu katika nia yako kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kupitia matumizi yako ya nia."

7_edited.png

Mungu Huwathamini Wanyonge

"Ni askari waliojeruhiwa pekee wanaoweza kutoa huduma katika huduma ya upendo—maumivu yako ni maandalizi ya huduma ya thamani kwa Yesu."

10_edited.png

Mungu Anakujali

"Kuweka wasiwasi wetu kwa Mungu ni unyenyekevu, wasiwasi usiofaa ni aina ya kiburi kisichotaka kumtegemea Yeye aliye na nguvu zote."

14_edited.jpg

Mfinyanzi Anapokuwa Kwa Ajili Yetu

"Je, kuna kitu kinachofariji zaidi kuliko ukweli kwamba Muumba yupo pamoja nasi? Kwa nguvu zake zote, yupo upande wetu!"

17_edited.png

Wanamapinduzi kwa Ajili ya Mwokozi

"Kristo ameanzisha mapinduzi dhidi ya ufalme wa Shetani, akiwaita watu wake kuwa wanamapinduzi wa wokovu."

20_edited.png

Kwanini Tushikilie Matumaini Yetu Kwa Uthabiti

"Inyooshe mikono yako na ushike kile ambacho umepewa na Kristo, na ukishikilie kwa nguvu zako zote — kama anavyofanya kazi kwa ukuu."

23_edited.png

Ahadi Bora zaidi ya Mungu

"Hakuna wakati ambapo ahadi ya Warumi 8:32 itakosa umuhimu. Ahadi hii haiwezi kushindwa."

26_edited.jpg

Huduma na Hofu ya Mwanadamu

"Uwepo na kibali cha Mungu ni vya thamani zaidi kuliko sifa za wanadamu—Yeye ndiye anayekuhifadhi na kukuokoa, na atakuwa pamoja nawe daima"

29_edited.png

Matokeo 10 ya Ufufuo wa Yesu

"Ufufuo wa Yesu ni msingi wa imani ya Kikristo, unatupatia uzima mpya, msamaha wa dhambi, Roho Mtakatifu, na uhakikisho wa wokovu."

32_edited.jpg

Akiita, Anatunza

"Maandiko yanaonyesha Mungu ni mwaminifu na atawahifadhi milele wale aliowaita, akifanya chochote ili tuendelee kumtumaini."

2_edited.png

Mzunguko wa Msamaha

"Yesu anafundisha kuwa Mungu alitusamehe tulipomwamini Kristo (Matendo 10:43), na kutokana na msamaha huo, tunawasamehe wengine."

5_edited.jpg

Madhumuni Makuu ya Huduma

"Jehanamu iko hatarini kati ya kurudi nyuma au kuvumilia. Tunaonyana: Usiyumbishwe, usitange mbali, usiipende dunia."

8_edited.jpg

Je, Unafurahi Kuwa Wewe Si Mungu?

"Ulimwengu uliumbwa ili tuustaajabu na kumtukuza Mungu, hili ndilo lengo na mwisho wa kuridhisha wa mambo yote."

11_edited.jpg

Aina Bora ya Utumwa

"Ubwana wa Yesu uko juu ya mabwana wote; ukombozi wetu upo salama.
Uhuru wetu una mipaka kwa rehema zake. Yesu ni Bwana wetu."

14_edited.jpg

Kristo kama Njia na Hatima

"Yesu Kristo ni ufunuo mkuu wa Mungu, na njia ya kufurahia utukufu wa Mungu kupitia wokovu. Bila Kristo, kusudi la ulimwengu lingeisha."

17_edited.jpg

Miundo Mizuri ya Mungu

"Ah, jinsi gani mipango ya Mungu ni tamu katika wokovu wa enzi wa wenye dhambi waliokosa tumaini na waliokauka mioyo!"

20_edited.jpg

Kushangazwa na Ufufuo

"Laana ya asili yetu ni kwamba tunachokifurahia huanza kuonekana kama kitu cha kawaida. Ukweli haujabadilika; sisi tumebadilika."

23_edited.jpg

Saa ya Tishio Lisilo la Kawaida

"Wakristo wengi ulimwenguni leo hawajui hatari ya kumwamini Kristo, 
tumezoea uhuru bila mateso, kana kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa."

26_edited.jpg

Mungu Anapokuwa Kwa Ajili Yetu 100%

"Kupitia imani ndani ya Kristo, ghadhabu ya Mungu iliondolewa na Mungu yupo kwa ajili yetu 100%."

1_edited.png

Faraja Yetu Inapotoka

Imejumuishwa katika Agano

4_edited.png

TUMAINI KWA WAKRISTO WASIO WAKAMILIFU 

“Kristo, leo nimefanya dhambi. Lakini naichukia dhambi yangu. Kwa maana umeandika sheria moyoni mwangu, na ninatamani kuifanya."

7_edited.png

NEEMA ILIYOKATALIWA NA ILIYOTOLEWA

“Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hukamilishwa katika udhaifu.”

10_edited.png

JINSI WAUMINI WATAKAVYO HUKUMIWA

"Mapungufu na makosa ya waumini yataonekana Siku ya Hukumu, lakini dhambi hizi zitaonyeshwa kama dhambi zilizosamehewa"

13_edited.png

AMRI INAYOTENGENEZA

"Njia ya kutii amri ya kuzaliwa ni kupata zawadi ya uhai na pumzi, kisha kumlilia Mungu kwa imani, shukrani, na upendo."

16_edited.png

MANENO YA UPEPO

"Kurejesha nafsi, sio kukemea kidonda, ni lengo la upendo wetu"

19_edited.png

JINSI YA KUMTUMIKIA BOSI MBAYA

"Paulo anasema kazi zetu zote zinapaswa kufanywa kama kazi kwa ajili ya Kristo, sio kwa msimamizi wa kibinadamu."

22_edited.png

Tutatawala Vitu Vyote

"Yesu anajaza ulimwengu kwa utawala wake tukufu kupitia sisi."

25_edited.png

KUCHELEWESHWA KWA UKOMBOZI

"Mungu huwaokoa watu wake kutokana na madhara fulani, sio yote. Hii inafariji kwani vinginevyo tunaweza kudhani ametusahau au ametukataa."

28_edited.png

JINSI YA KUTUBU

"Hisia mbaya zisizoeleweka kwamba wewe ni mtu mbaya si sawa na kuhukumiwa kwa dhambi. Kuhisi kuoza sio toba."

31_edited.png

MAKUSUDI MATANO YA MATESO

"Mateso haya ya muda mfupi yanatuandalia uzito wa milele wa utukufu usio na kifani."

21.png


"Lengo letu ni kutumainia upendo wake thabiti. Kumkimbilia. Kumfurahia Mungu, kumthamini na kufurahia ushirika na kibali chake."

 

24.png


"Hii ni njia ya kumpa kisasi Yeye ambaye kinamhusu. Kisasi ni changu, asema Bwana. Unakiweka chini. Nitakichukua. Haki itatendeka."

 

27.png

"Kwa Mungu, sifa ni mwangwi mzuri wa ubora wake katika mioyo ya watu wake.
Kwetu sisi, sifa ni kilele cha kuridhika kinachotokana na kuishi katika ushirika na Mungu."

30.png


"Tunamwomba Mungu atufanyie sisi kwa njia ya Kristo yale ambayo hatuwezi kujifanyia wenyewe—kuzaa matunda."

33.png

"Mungu atawaponya kwa kuwanyenyekeza. Atamponya mgonjwa kwa kukiponda kiburi chake."
 

36.png


"Viwanda vikubwa na mishahara mikubwa ni ukweli wa nyakati zetu, na si lazima iwe mbaya. Ubaya ni kudhani mshahara mkubwa lazima uambatane na maisha ya kifahari."
 

39.png

"Basi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe!"
 

42.png

"Mungu anatuita tusikie Neno lake la mwisho, la uamuzi, lisilokoma — kulitafakari, kulisoma, kulihifadhi akilini, kulikawia, na kulifikiria hadi litujaze kabisa ndani ya nafsi zetu."
 

45.png

"“Mambo yote yanawezekana kwa Mungu!” — mbele maneno hayo yanatoa tumaini, na nyuma yanatoa unyenyekevu. Hayo ni tiba ya kukata tamaa na tiba ya kiburi — dawa kamili ya wamishonari."

48.png

"Hivyo, mateso yote yanayokuja katika njia ya utii ni mateso pamoja na Kristo na kwa ajili ya Kristo — iwe ni saratani ukiwa nyumbani au kuteswa ukiwa mbali."

18.png

"Mungu kamwe hawi mwathirika wa hali. Yeye halazimishwi kamwe katika hali ya kulazimishwa kufanya kitu ambacho hawezi kukifurahia. Yeye hadhihakiwi. Yeye habanwi, hapingwi wala kulazimishwa."

21.png

"Tofauti kuu ni kwamba: 
(1) Masihi, Yesu, amekuja na kumwaga damu ya agano jipya kwa wokovu wa wote; 
(2) agano la kale haliwatawali watu wa agano jipya la Mungu; na 
(3) moyo mpya na nguvu ya Roho Mtakatifu imetolewa kwa njia ya imani."

24.png

"Kwa hiyo mantiki ya kutoogopa katika uso wa dhiki ni ukweli huu maradufu: Shida yako na imani yako katika uso wa dhiki ni zawadi za Mungu."

27.png


"Tunapambana na mahangaiko kwa kupigana na kutokuamini na kupigania imani katika neema ya wakati ujao."

 

30.png


"Kila siku ina shida zake. Lakini kamwe si zaidi ya unavyoweza kustahimili kwa neema Yake." 
 

33.png


"Furaha yetu haiinuki tu kutoka katika mtazamo wa kipindi cha nyuma kwa shukrani. Huinuka pia kutoka katika mtazamo wa mbele kwa matumaini"

36.png

"Katika Yesu Kristo sisi tuliozaliwa na Mungu tunayo fursa isiyoelezeka ya kumjua Yehova kama Baba yetu - MIMI NIKO AMBAYE NIKO - Mungu."

39.png


"Je, tujikane wenyewe na kuwapenda wengine kama Mungu anavyotupenda sisi na kuhatarisha mali na maisha yetu? Au tubaki "salama" ?" 
 

42.png


"Maisha yetu ya kimwili yanaumbwa na kudumisha na neno la Mungu, na maisha yetu ya kiroho yanahuishwa na kudumishwa na neno la Mungu." 
 

45.png


"Nia ya Mungu ni kukuza utimilifu wa utukufu wake kwa kumwaga rehema kwetu - kwetu sisi wenye dhambi, ambao tunamhitaji sana."
 

14.png

Udhaifu Wetu Unadhihirisha Ustahili Wake

Kuishi kwa imani katika neema ya Mungu kunamaanisha kuridhika na yote ambayo Mungu ni kwa ajili yetu ndani Yesu Kristo. 

17.png

Salama Kadri Mungu Alivyo Mwaminifu

Hizi ni ahadi za Mungu wetu asiyeweza kusema uongo. Wale waliozaliwa mara ya pili wako salama kama vile Mungu alivyo mwaminifu.

20.png

Lengo la Uumbaji

Mungu alituumba ili tumjue na kumpenda na kumwonyesha. Na kisha akatupa dokezo la jinsi alivyo: ulimwengu.
 

23.png

Unirehemu, Ee Mungu

Leo inamaanisha kugeuka, ukiwa bila msaada, kwa Kristo, ambaye damu yake inalinda rehema zote tunazohitaji.

26.png

Mifano Mitatu ya Jinsi Imani Inavyotimiza Maazimio Mema

Mungu na aongeze imani yetu ya kila siku katika ahadi za thamani za Mungu — ahadi za neema yake ya baadaye isiyokoma, iliyopatikana kwa damu, inayomtukuza Kristo.

29.png

Unakubali Kushindwa na Dhambi ya Zinaa, Kwasababu...

Watu wanakubali kushindwa na dhambi za kingono kwa sababu hawana utimilifu wa furaha na shangwe katika Kristo. 

32.png

Maana ya Ufufuo kwa ajili Yetu

Ufufuo ni ahadi ya Mungu kwamba wote wanaomwamini Yesu watakuwa wanufaika wa nguvu za Mungu za kutuongoza katika njia za haki na katika bonde la mauti.

35.png

Kufurahia Kusifu


Mungu yu upande wetu! Na msingi wa upendo huu ni kwamba Mungu amekuwa, yuko sasa, na atakuwa milele upande wake mwenyewe.

38.png

Pale Upendo wa Mungu Unapokuwa Mtamu Zaidi

Upendo usio na masharti ni chanzo na msingi wa mabadiliko ya kibinadamu yanayofanya uwezekano wa upendo wenye masharti kuwa mtamu. 

41.png

Kusamehewa kwa ajili ya Yesu

Heshima isiyo na kikomo ambayo Baba anayo kwa Mwana hufanya iwezekane kwangu, mtenda dhambi mwovu, kupendwa na kukubalika ndani ya Mwana, kwa sababu katika kifo chake alithibitisha thamani 
na utukufu wa Baba yake.

44.png

Simba na MwanaKondoo

Huu ndio utukufu wa kipekee wa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliyefanyika mwili -mchanganyiko wa kushangaza wa ukuu na unyenyekevu.

12.png

Habari Njema: Mungu Ana Furaha

“Ikiwa Mungu hana furaha, basi lengo la injili—kukaa na Mungu milele—si lengo lenye furaha, na hivyo injili hiyo isingekuwa injili hata kidogo. ”

 

15-min.png

“Kristo alishinda uchungu na kisasi kwa imani katika ahadi za Mungu, Hakimu mwema. Je, sisi tunapaswa kufanya nini zaidi, kwa kuwa tuna haki ndogo ya kunung'unika kwa kuteswa kuliko yeye?”

18.png

“Biblia inatupa mtazamo wa kustaajabisha katika nafsi ya Yesu usiku kabla ya kusulubiwa kwake. Tazama na ujifunze kutokana na jinsi Yesu alivyopigana vita vyake vya kimkakati dhidi ya kukata tamaa au sonona.”

21.png


“Lakini imani katika neema ya wakati ujao huzaa upendo kwa kuondoa hatia na hofu na uchoyo kutoka moyoni.”

 

24.png


“Neema ndiye mwamuzi mkuu katika huduma ya Paulo, ikimpa nguvu ya kutekeleza kazi yake.”
 

27.png

“Kusudi la karama za kiroho ni kupokea na kusambaza neema ya Mungu ya wakati ujao kwa mahitaji hayo.”
 

30.png

““Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.” Tunajihubiria hivyo. Na tunaitupa kwenye uso wa Shetani. Na tunaiamini.”

33.png

“Kwa hivyo, kazi kuu ya Shetani ni kutetea, kukuza, kusaidia, kutisha, na kuthibitisha mwelekeo wetu wa kutenda dhambi. Na kutuonda katika imani na kutuzuia kutubu.”

36-min.png

“Majanga yote makubwa duniani yanaweza kuua mwili tu. Lakini tusipopigana na tamaa, tunapoteza nafsi zetu. Milele.”
 

39-min.png

“Kusudi moja yapo la kutikiswa na kuteseka ni kufanya imani zetu zisitikisike zaidi.”

9.png

Wana wa Ibrahimu Ni Kina Nani?

“Ninyi mnaomtumainia Yesu Kristo na kumfuata katika utiifu wa imani ni wazao wa Ibrahimu na warithi wa ahadi zake za agano.”
 

12.png

Mwaminifu Katika Mambo ya Kawaida


“Maisha ya imani ni kioo kikuu cha uaminifu wa Mungu.”
 

15.png

Mtukuze Mungu katika Mwili Wako


“Unao mwili. Lakini sio wako. “Mlinunuliwa kwa gharama kubwa. Basi mtukuzeni Mungu katika miili yenu.” ”
 

18.png

Imani kwa ajili ya Wakati Ujao


“Ujasiri kwamba wema huu utadumu milele unategemea neema ya Mungu iliyotolewa hapo awali, hasa kupitia Mungu kumtoa Mwana wake kwa ajili yetu.”
 

21.png

Ni Kwa Kiasi Gani Mungu Anataka Akubariki

“Mungu hasiriki kirahisi; hasira yake haina mwako wa haraka. Ana nguvu na shauku isiyo na kikomo kutimiza anavyofurahia.”

24.png

Ni Maombi ya Namna Gani Humpendeza Mungu?

“Alama ya kwanza ya wanyoofu, ambao sala zao zinampendeza Mungu, ni kutetemeka chini ya neno la Mungu. Hawa ndio anaowatazama Bwana.”

27.png

Neema ni Msamaha - na Nguvu!

“Neema ni karama na uwezo wa Mungu wa kutotenda dhambi. Neema ni nguvu, sio msamaha tu.”
 

30.png

Imani Humheshimu Yule Inayomwamini

“[Imani] humheshimu yule inayemwamini kwa heshima ya juu zaidi, kwa kuwa inamwona kuwa mkweli na mwaminifu.”
 

33.png

Hofu Inayotuvutia  Ndani

"Kile tunachopaswa kuogopa si kuamini, bali kutokuwa na imani. Hofu kumkimbia Mungu, lakini tukitembea naye, atakuwa rafiki na mlinzi wetu milele."

36.png

Mzizi Imara wa Upendo wa Kivitendo

"Mungu mkuu wa neema hutimiza ahadi zake kwa wanaomtumaini, akionyesha uzuri na utoshelevu wake, na kutupa nguvu ya kupenda kwa vitendo."

7.png

Mungu Anaudhihirisha Upendo Wake

"Kwa maneno mengine, lengo la kila jambo ambalo Mungu anatupitisha ni tumaini. Anataka tuwe na tumaini lisiloyumbayumba katika dhiki zote."

10.png

Vyanzo Saba Vya Furaha


"Maisha ya furaha katika Roho Mtakatifu ni maisha ya kiungu yapitayo uzoefu wa kawaida."

 

13.png

Kuridhika na Maagizo Yake

"Imani inayoshinda uadui wetu kwa Mungu hutuweka huru kuzishika amri zake na kusema kama mtunga-zaburi, “Kufanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu.”"

16.png

Nenda kwenye Karamu ya Bwana


"Unasema hujaonja utukufu wa Mungu. Ninasema, umeonja vichamgamsha kinywa. Nenda kwenye chakula. Nenda kwa Mungu mwenyewe."
 

19.png

Mawazo Yana Athari

"Mawazo yana matokeo. Kwa hivyo, na tuweke mawazo yetu yote chini ya mamlaka ya neno la Mungu."

22.png

Hatari Tano za Kidigitali


"Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msitoe nafasi ya mwili hata kuridhisha tamaa zake."

25.png

Jinsi ya Kuchukia Maisha Yako

"Yeyote anayechukia maisha yake katika ulimwengu huu atayaweka hata uzima wa milele."

28.png

Je, Kristo Anastahili?

"Ina maana ya kwamba tunapoketi kuhesabu gharama ya kumfuata Yesu - tunapopima yaliyo "mabaya" na yaliyo"bora" - yeye anastahili. Anastahili sana."

31.png

Nguvu ya Kusubiri kwa Uvumilivu


"Uvumilivu unaonyesha nguvu ya ndani, huku wasio na subira wakitegemea usaidizi wa nje kutokana na udhaifu wao."

34.png

Mungu Anapoenda Kinyume Na Mapenzi Yake


"Wewe huyaoni makusudi haya sasa. Niamini. Najua ninachofanya. Nakupenda."

4.png

Mahitaji Yetu Mawili ya Muhimu Zaidi

"Kila mmoja wetu ana haja ya kuokolewa na kusaidiwa, kwa upande mmoja, na haja ya kusudi na maana, kwa upande mwingine."

7.png

Mungu Hututia Nguvu Kupitia Wengine

"Yesu aliwatunza wale kumi kwa kumtunza Petro. Aliyeimarishwa anakuwa mwenye kuimarisha."

10.png

Maana Ya Kumuombea Adui Yako

"Kuombea adui zako ni aina ya upendo mkuu, ukitamani mema, wokovu, na furaha yao ya milele."

13.png

Aibu Iliyowekwa Vizuri ni Ipi?

"Kigezo cha kibiblia cha aibu inayofaa kinasema, Jisikie aibu kwa kushiriki katika chochote kinachomdhalilisha Mungu."
 

16.png

Zungumza na Machozi Yako

"Ikiwa tutakula majira ya baridi yajayo, lazima tutoke kwenda shambani na kupanda mbegu, iwe tunalia au la."

19.png

Rehema kwa ajili ya Leo

"Rehema za leo ni za shida za leo. Rehema za kesho ni za shida za kesho."
 

22.png

Kesho Njema kwa Walioshindwa

"Hii ndiyo Injili: Ingawa mmefanya dhambi na kumwaibisha Bwana, na ingawa mlichagua kujitawala kwa dhambi, bado kuna tumaini na rehema."

25.png

Sababu Tano za Kutokuwa na hofu


"Tukimuona Mungu ni wa thamani kwa namna hii, hatutakuwa na hofu na Mungu ataabudiwa."
 

28.png

Wokovu wa Paulo Ulikuwa Kwa Ajili Yako

"Mungu alikuwa anakuwaza wewe alipomchagua Paulo na kumwokoa kwa neema yake kuu kama alivyofanya."

31.png

Mabadilishano Makuu

"Hatuwezi kusisitiza vya kutosha kwamba Kristo ni jibu la Mungu kwa tatizo letu kubwa zaidi. Yote ni kwa sababu ya Kristo."

2_edited.png

Faraja Yetu Inapotoka

"Pilato ana mamlaka. Herode ana mamlaka. Wanajeshi wana mamlaka. Shetani ana mamlaka. Lakini hakuna aliye na mamlaka huru, ya kujitegemea."
 

5_edited.png

Mungu anafurahia kukutendea mema

"Mungu hafanyi mema kwa watoto wake kwa kusitasita—ni furaha yake kuu kututendea mema daima!"

8_edited.jpg

Ninawezaje Kujazwa na Roho?

"Ni neno la ahadi linalotujaza tumaini, linalotupa furaha inayofurika kwa nguvu na uhuru wa kumpenda jirani yetu."

12_edited.jpg

Tumwabudu MwanaKondoo

"Tunamheshimu na kumwabudu Kristo kwa maombi yetu duniani, tukifurahia kwamba yatatolewa mbinguni kama uvumba wenye harufu nzuri."

15_edited.jpg

Yesu ni Amina ya Mungu

"Tunamheshimu na kumwabudu Kristo kwa maombi yetu duniani, "Katika Yesu Kristo, Mungu anasema Ndiyo yake kwetu kupitia ahadi zake; na katika Kristo tunasema Ndiyo yetu kwa Mungu kupitia maombi." 

18_edited.jpg

Yesu Atamaliza Kazi

"Misheni haiwezi kushindwa, kwa maana Kristo, anayetengeneza siku zijazo, ameahidi: ‘Injili hii ya ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote."

21_edited.jpg

Muhtasari wa Injili kwa hoja Sita

"Kristo pia aliteseka mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili ya wasio haki, ili atulete kwa Mungu."

24_edited.png

Duka la Peremende za Shetani

"Kristo aliteseka na kufa kunikomboa, kwa hiyo nimekufa kwa dhambi. Alikufa kununua kitu cha thamani zaidi kuliko raha za dhambi."

27_edited.png

Kutosheka Milele

"Yesu ndiye mwisho wa safari yetu ya kutosheka—hakuna kitu zaidi, na hakuna kilicho bora zaidi."

30_edited.png

Pale Wote Watakapokuacha

"Unapoachwa na marafiki, Je, unalia dhidi ya Mungu au unapata ujasiri katika ukweli kwamba Mungu yuko pamoja nawe daima?"

33_edited.jpg

Nini Hufunga Mikono ya Upendo?

"Tatizo la kanisa leo si shauku ya kwenda mbinguni, bali ni Wakristo kutumia muda kidogo kusoma Maandiko na muda mwingi kutafuta pesa."

3_edited.png

Upendo Mkuu

"Mungu anatupenda kwa kutuonyesha ukuu wake, si kwa kutufanya kuwa wakuu. Kufika mbinguni na kujiona sisi  kuwa wakuu ingekuwa huzuni kuu"

6_edited.png

Kutukanwa Hapa, Kulipwa Kule

"Mtunga-zaburi anaposema, “Katika yote ayatendayo hufanikiwa,” anaelekezea kwenye maisha baada ya kifo, ambapo ustawi wa kweli utaonekana."

9_edited.jpg

Bora Kuliko Pesa, Ngono na Mamlaka

"Ngono, pesa, na mamlaka ni taswira hafifu ya kweli na raha za juu zaidi zitakazovifanya hivi kuonekana kama miayo."

12_edited.jpg

Riziki ya  Lincoln

"Ni jambo la kushangaza jinsi mateso ya kibinafsi na ya kitaifa yalivyomvuta Lincoln katika ukweli wa Mungu, badala ya kumsukuma mbali."

15_edited.jpg

Kila Hatua ya Kalvari Ilikuwa ya Upendo

"Kila hatua kwenye barabara ya Kalvari ilimaanisha, “Nakupenda.”"

18_edited.jpg

Wakati Wewe Huwezi Kufa

"Wewe pia una ushuhuda wa mwisho wa kutoa, na hautakufa mpaka uutoe."

21_edited.jpg

Mtumishi wetu, Yesu

"Haimvunjii heshima kusema kwamba yeye peke yake ndiye anayeweza kutuhudumia kwa kile tunachohitaji zaidi."

24_edited.jpg

Mungu Hufungua Moyo

"Ikiwa wewe ni muumini wa Yesu: Uliteuliwa kuamini, ulipewa kutubu, na Bwana akafungua moyo wako."

27_edited.jpg

Athari Kali za Ufufuo

"Tumaini la ufufuo lilibadili maisha ya Paulo, likimkomboa kutoka kupenda mali na ulaji, na kumwezesha kuishi bila starehe zisizo za lazima"

2_edited.png

MAANA YA KIFO CHA YESU KWA KIFO CHETU

"Tatizo kuu maishani mwako ni upatanisho na Mungu. Kifo cha Kristo ni dhabihu ya kubeba dhambi zetu, alizibeba na kufa kifo tulichostahili"

5_edited.png

ADUI YETU ASIYE NA MENO

Shetani anaweza kutuumiza kimwili na kihisia—hata kutuua. Anaweza kutujaribu na kuwachochea wengine dhidi yetu. Lakini hawezi kutuangamiza.

8_edited.png

PATA USICHOWEZA KUPOTEZA

"Yeye sio mpumbavu ambaye hutoa asichoweza kuhifadhi ili kupata kile ambacho hawezi kupoteza."

11_edited.png

SHAUKU KWA AJILI YA MUNGU NA UKWELI

"Kutojali ukweli ni kutojali kuhusu Mungu. Kumpenda Mungu kwashauku ni kupenda ukweli kwa shauku kubwa."

14_edited.png

DIRISHA LA MOYO

"Akili ni dirisha la moyo. Tukiacha akili zetu zidumu kwenye giza, moyo utahisi giza.  Tukifungua  akili zetu kwa nuru, moyo utahisi mwanga"

17_edited.png

Imani ya Kweli Ina shauku ya Kuja kwa Kristo

"Kumtarajia Kristo kwa shauku ni ishara tu kwamba tunampenda na kumwamini — tunamwamini kweli kweli."

20_edited.png

VITA VYA KUKUMBUSHA

"Pasipo kukumbuka ukuu, neema, nguvu, na hekima ya Mungu, tunaingia katika hali ya kukata tamaa inayoumiza."

23_edited.jpg

Nenda moja kwa moja kwa Mungu

"Yesu anasema unaweza kwenda kwa Baba moja kwa moja kwani “Baba mwenyewe anawapenda ninyi.”

26_edited.png

MTOAJI ANATAPA UTUKUFU

"Ni habari njema sana kwamba Mungu anatengeneza utukufu wake ukuzwe kupitia matumizi ya neema yake."

29_edited.png

IMESABABISHA KURUDI

"Hakuna matumaini kwa watu wa Mungu isipokuwa Mungu awaongoze kutoka katika kuteleza na kurukaruka katika dhambi na kutokuamini."

22.png

"Mungu hatuhitaji sisi, bali kujitosheleza kwake kusiko na kikomo kumemwagika kwa upendo kwetu wenye dhambi tunaomhitaji yeye, na zawadi ya nafsi yake katika Yesu"

25.png


"Ikiwa Mungu hana furaha, basi lengo la injili si lengo la furaha, na hiyo inamaanisha kuwa isingekuwa injili hata kidogo."
 

28.png

"Kifo cha Kristo ni hekima ya Mungu kwamba upendo wa Mungu huwaokoa wenye dhambi kutoka katika ghadhabu ya Mungu, huku ukishikilia na kudhihirisha haki ya Mungu katika Kristo."

31.png

"Hatumtukuzi Mungu kwa kumhudumia mahitaji yake, bali kwa kuomba atutimizie yetu, kutumaini atajibu, na kuishi kwa furaha tunakijitoa kwa upendo kwa wengine."

34.png

"Hatuombi si kwasababu hatutaki kuomba. Hatuombi kwasababu hatupangi kuomba. Matokeo ya kutokupanga kuomba ni kurudia yale yale ya zamani."

37.png

"Unapompenda mtu ambaye Mungu amekufanya kuwa mwili mmoja, unajipenda mwenyewe. Yaani furaha yako kuu inapatikana katika kutafuta furaha kuu ya mwenzi wako."
 

40.png

"Alipanga ndoa kwa makusudi sana ifanane na uhusiano kati ya Mwanawe na kanisa, ambao alikuwa ameupanga tangu milele."
 

43.png

"Yesu uhusiana na mungu namna ambavyo miali au mng'ao uhusiana na utukufu,  au namna ambavyo miali ya mwanga wa jua uhusiana na jua."
 

46.png

"Kama furaha yako ni kupata neema ya Mungu inayokujaza na kumwagika kwa manufaa ya wengine, Mungu atafanya yasiyowezekana kupitia wewe kwa ajili ya wokovu wa watu ambao hawajafikiwa."

49.png


"Maisha ya dunia hii si ziwa, ni mto unaotiririka kuelekea uharibifu. Usipomsikiliza Yesu kwa bidii na kumtazama kila saa, hutosimama ulipo, utarudi nyuma na kuelea mbali na Kristo."

19.png

"Ni uhuru wa kushangaza na kutokuwa na masharti kwa neema ya uteuzi — ikifuatiwa na kazi zote nyingine za neema ya wokovu — vinavyoturuhusu kuchukua na kuonja zawadi hizo kama zetu wenyewe bila kujikweza."

22.png


"Je, furaha kuu zaidi inayomtukuza Kristo haipatikani kwa kumtazama Yesu siku nzima na kupaza sauti, “Wewe ni wa ajabu!” “Wewe ni wa ajabu!""

 

25.png


"Kumlipa Bwana ni kuendelea kupokea kutoka kwake ili wema wake utukuzwe. Kuinua kikombe cha wokovu kunamaanisha kuunywa wokovu wa Bwana huku ukitarajia zaidi."

 

28.png

"Zaidi ya hayo, haijalishi nini kitatokea, Mungu atafufua mwili wako siku moja na kuhifadhi maisha na mwili wako kwa ushirika wake wa milele."

31.png


"Tunapaswa kupigana na kutokuamini kwa wasiwasi kwa kutumia ahadi za neema ya wakati ujao."
 

34.png


Ninamshukuru Mungu kwamba tena na tena ameuamsha moyo wangu kumtamani, kumwona, na kuketi kwenye karamu ya Furaha ya Kikristo na kumwabudu Mfalme wa Utukufu."

37.png


"Kujitolea maisha kwa starehe za kimwili, usalama, na msisimko ni kama kutupa pesa kwenye shimo la panya." 

40.png


"Ina maana kwamba inapokuja suala la kuwa mtarajiwa wa neema, historia yako haina uhusiano wowote na chaguo la Mungu. Hiyo ni habari njema."

43.png

"Geuka kutoka dhambini na umtumaini Bwana Yesu Kristo; na uweza wa Mungu Mwenyezi utakuwa heshima ya roho yako, malipo ya maadui zako, na kimbilio la maisha yako — milele."

46.png


"Kutokuamini ahadi za Mungu ni mzizi wa wasiwasi, ambao, kwa upande wake, ni mzizi wa dhambi nyingine nyingi."
 

15.png

Usiogope Kifo Tena


Kwa hiyo, tuko huru kutokana na hofu ya kifo. Mungu ametuhesabia haki. Kuna neema ya baadaye tu mbele yetu.
 

18.png

Maana 10 Za “Yahweh”

Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
 

21.png

Mtawala wa Asili Yote

Kuishi kwa imani katika neema ya Mungu kunamaanisha kuridhika na yote ambayo Mungu ni kwa ajili yetu ndani Yesu Kristo. 

24.png

Nyakati Tofauti za Neema

Neema ni nguvu inayofanya kazi, iliyopo sasa, inayobadilisha, na kuwezesha utii.

27.png

Mungu Husamehe na Bado Ni Mwenye Haki


Hivyo Mungu anadumisha haki yake kamilifu na wakati huo huo akionyesha rehema kwa wale wanaomwamini Yesu, bila kujali ni dhambi ngapi au ni za kutisha kiasi gani.  

 

30.png

Maana Ya Kumhimidi Bwana


Inamaanisha kuzungumza vizuri kuhusu ukuu na wema wake — na kumaanisha  kwa dhati kutoka ndani kabisa ya nafsi yako.
 

33.png

Yesu Ndiye Unayemtafuta

Lazima tuwe na kitu halisi. Lazima tuone Asili ya nguvu zote na wema wote na kusudi zote. Ni lazima tumwone na kumwabudu Kristo aliyefufuka.

36.png

Mungu Si Mwabudu Sanamu

Badala yake, ni lazima tuone kwamba Mungu ni upendo kwa sababu anafuatilia bila kuchoka sifa za jina lake katika mioyo ya watu wake.

39.png

Vivuli na Vijito


Mwisho wa yote, haitakuwa bahari au milima au mabonde au buibui wa maji au mawingu au galaksi kubwa ambazo zitajaza mioyo yetu na mshangao na kujaza vinywa vyetu na sifa za milele. Itakuwa ni Mungu mwenyewe.

42.png

Mambo Sita Yanayomaanisha Kuwa Ndani Ya Kristo Yesu

Ninaomba kwamba kamwe usichoke kuchunguza na kushangilia upendeleo usiokwisha wa kuwa “ndani ya Kristo Yesu.”
 

10.png

Furaha Ya Mungu Kukutendea Mema


“Msiogope, enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi ufalme.”
 

13.png


"Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”

 

16.png


“Mateso ya Kristo yalikuwa malipo ya Mungu kwa maumivu yote uliopata kutoka kwa Mkristo mwenzako. Ukristo haupunguzi uzito wa dhambi wala hauongezi matusi kwa majeraha yetu.”
 

19.png

“Moyo wa imani ni tofauti kabisa. Tamaa zake zinaendelea kuwa kali ukitazamia siku zijazo. Lakini, kile Unachotamani ni kuridhika kikamilifu kwa kupata yote ambayo Mungu ni kwa ajili yetu kupitia Yesu.”

22.png

Nini Kinakusukuma kwenye Utumishi?

“Apandaye kwa mwili, katika mwili wake atavuna uharibifu; lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.”
 

25.png

“Nguvu tunazohitaji sasa 
na katika miongo ijayo zinatoka kwa Kristo mwenye nguvu, ambaye daima yupo kutenda kwa ajili ya mapenzi yake mema.”

28.png

“Maombi ni aina ya imani inayotuunganisha leo na neema ambayo itatufanya tuwe na uwezo wa huduma ya kesho. Kuzigatia muda ni  muhimu sana.”
 

31.png

“Vita dhidi ya kukata tamaa ni vita ya kuamini ahadi za Mungu. Na imani hiyo katika neema ya Mungu ya wakati ujao inakuja kwa kusikia neno. Na hivyo kujihubiria neno la Mungu ni kiini cha vita.”

34.png

“Kwa hivyo, kazi kuu ya Shetani ni kutetea, kukuza, kusaidia, kutisha, na kuthibitisha mwelekeo wetu wa kutenda dhambi. Na kutuonda katika imani na kutuzuia kutubu.”

37-min.png


“Hafi moyo kwa sababu utu wake wa ndani unafanywa upya.”

40-min.png

“Ukidhani mateso yako hayana maana, utajitenga na Mungu. Ni muhimu kuamini kwamba Mungu hutoa neema kupitia mateso.”
 

10.png

Imani kwa ajili ya Yasiyowezekana

“Hii ndiyo imani tunayotakiwa kuwa nayo, kwamba Mungu atatufanyia kile tusichoweza kujifanyia.”
 

13.png

Wote Wana Uadui na Mungu

“Uhasama huo ni dhidi ya Mungu wa kweli, lakini watu humfikiria kwa namna wanavyomtaka awe na mara chache huzingatia uwezekano wa kuwa hatarini mbele yake.”

16.png

Maombi ni kwa ajili ya Wenye Dhambi

“Sisi ni wenye dhambi na sisi ni ombaomba. Na tukiitambua dhambi hii, kuikataa, kuipiga vita, na kushikamana na msalaba wa Kristo kama tumaini letu, basi Mungu atatusikia na kujibu maombi yetu.”

19.png

Nisaidie Kutokuamini Kwangu

““Ee Bwana, asante kwa imani yangu. Idumishe. Itie nguvu. Iwe na kina zaidi. Usiiruhusu ishindwe. Ifanye kuwa nguvu ya maisha yangu, ili kwamba katika kila jambo ninalolifanya, upate utukufu kama Mpaji mkuu. 
Amina.””

22.png

Fungate Lisiloisha Kamwe

“Kwa Mungu, fungate haina mwisho. Yeye hana mwisho katika uwezo na hekima na ubunifu ili kusiwe na kuchoka kwa enzi trilioni za milenia zijazo.”

25.png

Jinsi ya Kuwaombea Wasioamini

“Mungu anafurahishwa na aina hii ya sala kwa sababu inampa haki na heshima ya kuwa Mungu aliye huru na mwenye enzi katika uchaguzi na wokovu.”
 

28.png

Utoshelevu Unaoshinda Dhambi


“Kiini cha imani ni kuridhika na yote ambayo Mungu ni kwa ajili yetu katika Kristo.”
 

31.png

Ninaweza Kuridhika Katika Kila Hali

"Imani katika ahadi hii— “Sitakuacha kamwe”—inavunja nguvu zote ambazo zinamvunjia Mungu heshima—tamaa zote. "
 

34.png

Maficho ya Wasiojiweza

"Tazama jinsi ulivyo tele wema wako, ambao ulionao. . . 
ukitenda kazi kwa ajili ya wale wakukimbiliao."

 

37.png

Msaada wa Mbingu katika Ghadhabu Inayokuja


"Itafika wakati uvumilivu wa Mungu utaisha."

 

8.png

Jinsi ya Kuomba Msamaha


"Mungu ni mwaminifu na mwenye haki, naye atakusamehe dhambi zako."

 

11.png

Ujuzi wa Kweli Huleta Furaha Kubwa Zaidi

"Furaha yetu lazima itokane na maarifa ya kweli ya utukufu wa Mungu ili kuakisi utukufu wake. Ili kumfurahia Mungu ipasavyo, ni lazima tumjue kweli."

14.png

Nini Maana ya Kumpenda Mungu

"Hiki ndicho kiini cha maana ya kumpenda Mungu: kutosheka ndani yake. Ndani yake — sio karama zake tu, bali Mungu mwenyewe, kama mtu mtukufu alivyo!"

17.png

Kwa Nini Tunapaswa Kuwapenda Adui Zetu

"Nguvu ya rehema ni kuridhika na rehema ya Mungu, ikilenga kumtukuza kwa kuwasaidia wengine wafanye hivyo, ili Mungu aonekane mkuu kwa mwanadamu kupitia upendo na rehema zake."

20.png

Upole Ni Nini?

"Tunaamini katika wakati wake na nguvu zake na neema yake kufanya mambo kwa njia bora zaidi kwa utukufu wake na kwa manufaa yetu."

23.png

Nuru Zaidi ya Nuru

"Kristo anajitoa kwetu kadri ya jinsi tunavyotaka burudisho kutoka kwake.  “Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote”"

26.png

Mungu Anafanya Kazi Kwa Ajili Yako

"Ukweli ulioje! Ni uhalisia ulioje! Mungu yuko macho usiku kucha na mchana kutwa kufanya kazi kwa ajili ya wale wanaomngoja."

29.png

Msingi wa Hakikisho Lako

"Uteule ndio msingi wa mwisho wa hakikisho letu kwa sababu, ni dhamira yake Mungu kuokoa, pia ni dhamira yake Mungu kuwezesha yote ambayo ni muhimu kwa ajili ya wokovu."

32.png

Imani Halisi Dhidi ya Imani Ya Udanganyifu

"Je, tunatamani kwa hamu kuja kwa Kristo? Au tunataka akae mbali, huku penzi letu na ulimwengu likiendelea?"

35.png

Kitu cha Kujivunia


"Kumtumikia Mungu ni kupokea, ni baraka, ni furaha, na ni faida." 

 

5.png

Bora Kuliko Kilimanjaro


"Ukiishi ndani ya ahadi hii kubwa, maisha yako ni imara na thabiti kuliko Mlima Kilimanjaro."

 

8.png

Vitabu Vitavyosomwa katika Hukumu

"Wokovu wake utahakikishwa kwa damu ya Kristo. Jina lake litakuwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyekufa."

11.png

Mfanye Shetani Ajue Kushindwa Kwake 

"Agano Jipya linafundisha kwamba kifo na ufufuo wa Kristo vilimshinda Shetani kabisa, na nguvu zake dhidi ya watu wa Mungu zimevunjwa."
 

14.png

Divai ya Mfalme Mkuu

"Kujifunza utii ni kukua na Mungu kupitia uzoefu wa utii na kujisalimisha kupitia mateso. Bila maumivu, hakuna mafanikio."

17.png

Omba kwa ajili ya Kujulikana Kwake


"Mungu anafurahia jina lake lijulikane na kuheshimiwa."

20.png

Kumkumbatia Yesu

"Imani ya kweli inamkumbatia Kristo kwa njia zozote ambazo Maandiko yanamshikilia kwa wenye dhambi maskini"
 

23.png

Kuogopa Kupotea

"Wema huu hauna mipaka, unadumu milele, na unajumuisha yote. Kuna wema pekee kwa wanaomcha. 
Kila kitu hufanya kazi kwa manufaa yao."

 

26.png

Tafuta Ustawi wa Jiji lako

"Tenda mema mahali Mungu alikokutuma kwa utukufu wake. Tuishi kwa matendo mema ili wenyeji watamani kumjua Mfalme wetu."
 

29.png

Uliumbwa kwa ajili ya Mungu

“Sisi ni watu wa Mungu kwa ajili ya jina lake. Kusudi letu ni kuutangaza utukufu wake.”

 

32.png

Siku Imekaribia

"Yesu alishinda dhambi na maumivu na kifo na Shetani alipokufa na kufufuka tena. Vita vya maamuzi vya vizazi vimekwisha. Ufalme umefika."
 

3_edited.png

Jivike silaha kupitia Ahadi hizi

"Kuwa na ahadi zinazofaa wakati wa majaribu ni ufunguo wa kushinda ahadi za dhambi kwa nguvu ya ahadi kuu ya Mungu."

 

6_edited.jpg

Mtazame Yesu kwa ajili ya Furaha Yako

"Mwasho wa kujipenda hutafuta kujiridhisha, lakini nafsi haikuundwa kujitosheleza."

9_edited.png

Fungua Madirisha ya Moyo Wako

"Kuwa na ahadi zinazofaa wakati wa majaribu ni ufunguo wa kushinda ahadi za dhambi kwa nguvu ya ahadi kuu ya Mungu."

13_edited.jpg

Kweli Mbili Zenye Nguvu na Upole Usio na Kifani

"Ukuu na rehema ya Mungu ni nguzo zisizoyumbishwa—tumaini langu la baadaye, nguvu yangu kwenye huduma, na tiba yaangu kwenye kukata tamaa."

16_edited.jpg

Ushindi Ni Hakika

"Ushindi huu ni hakika kwa sababu Mungu ndiye anayeufanya. Kwa hiyo tunaweza kuwa na uhakika."

19_edited.png

UHAKIKA wa Maombi

"“Amina” inamaanisha, “Ndiyo, Mungu ametoa ahadi hizi zote.” Inathibitisha uwezo, hekima, huruma, na neema ya Mungu."

22_edited.png

Yesu Alikufa kwa Ajili ya Wakati Huu

"Injili ya Yesu Kristo inang'aa zaidi—‘aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu’. Nilihitaji Mwokozi, na Yesu pekee ndiye anayefaa."

25_edited.png

Ujinga Unapelekea Kutokumcha Mungu

"Soma, tafakari, na jadili ukweli wa Mungu, kwani kutomjua Mungu huhakikisha kutomcha Mungu."

28_edited.jpg

Jinsi ya Kufurahia Neno la Mungu

"Usipunguze Ukristo kuwa madai na maazimio—ni suala la kile tunachopenda, kile tunachofurahia, na kile chenye ladha nzuri kwa roho zetu."

31_edited.png

NI HAKIKA kama upendo wa Mungu kwa Mwana wake

"Kuna maumivu na vikwazo maishani, lakini naamini Mungu hupunguza uharibifu wa changamoto hizi ili kuongeza furaha yangu ndani yake."

1_edited.jpg

Imejumuishwa katika Agano

"Yeyote anayekuja kwa Mungu kupitia Yesu Kristo akiwa na kiu ya kile Mungu alicho ndani ya Kristo, Mungu atafanya agano naye."

4_edited.png

Njia Tano Ambazo Mateso Husaidia

"Mateso hutulazimisha kumtegemea Mungu zaidi, Hutufanya tuwe karibu na lengo la neno lake, huku yakifisha tamaa za kimwili."

7_edited.jpg

Mafanikio Ya Dakika Za Mwisho

"Jipe moyo, mpiganaji. Endelea kuuliza, kutafuta, na kumwangalia Kristo. Mungu ana makusudi kwa kuchelewesha mafanikio yako."

10_edited.jpg

Imani Inayookoa Hairidhiki kwa Urahisi

"Watu wengi hudhoofisha imani iokoayo kwa kuiona kama uamuzi tu, bila mabadiliko ya tamaa na malengo."

13_edited.jpg

Mji Mzuri

"Mji wa Mungu utakuwa mkamilifu na utajawa na mema, matakatifu, mazuri, amani, kweli, na furaha kwasababu ya Uwepo wa Mungu."

16_edited.jpg

Wakati Utiifu Unapoonekana Kutowezekana

"Kwa wengi wenu, utii huhisi kama mwisho wa ndoto, ukihisi kuwa kumfuata Mungu kutaleta huzuni, na Mungu hawezi kubadilisha yote kwa mema"

19_edited.jpg

Aina ya Baridi Inayouaa

"Mungu anasema, “Iwe joto, baridi, juu, chini, ukali, ubutu, sauti kubwa, tulivu, angavu, giza . . . usicheze na mimi. Mimi ni Mungu."

22_edited.jpg

Kufurahia Utimilifu Wake

"Kutoka kwa utimilifu wa Neno, tunapokea neema isiyo na kikomo"

25_edited.png

Unapendwa Sana

"Ukimwona Yesu kama hazina yako kuu na kumpokea, unapendwa sana na Muumba wa ulimwengu."

28_edited.png

Tumehesabiwa Haki Kikamilifu

"Mungu akikusamehe na kukutangaza mwadilifu, hakuna rufaa au makosa yanayoweza kutafutwa dhidi yako."

3_edited.png

IMANI NDOGO KULIKO ZOTE

"Yote tutakayopata kutoka kwa Mungu mwaka huu, kama waumini katika Yesu, ni rehema, iwe raha au maumivu."

6_edited.png

MAPENZI YA MUNGU NI KWAMBA UMKARIBIE

"Haya ni mapenzi ya Mungu kwako, hata unaposoma haya maandishi. Hii ndiyo sababu ya kifo cha Kristo: ili umkaribie Mungu."

9_edited.png

MUDA KIDOGO TU

"Mungu ni "Mungu wa neema yote," akijumuisha hazina isiyo na kikomo ya neema ya wakati ujao tunayoihitaji kuvumilia hadi mwisho."

12_edited.png

UFUNGUO WA UZOEFU

"Njia ya kutii amri ya kuzaliwa ni kupata zawadi ya uhai na pumzi, kisha kumlilia Mungu kwa imani, shukrani, na upendo."

15_edited.png

UHURU WA NEEMA

"Tendo gani lingekuwa la upande mmoja zaidi, na lisilohitaji maelewano kuliko mtu mmoja kumfufua mwingine kutoka kwa wafu! Hii ndio neema!"

18_edited.png

DAWA YA KIBURI

"Kiburi hakiwezi kustahimili ushirika wa karibu wa Mungu katika kuendesha ulimwengu na maisha ya kila siku."

21_edited.png

NANGA YA FURAHA

"Furahini katika hili: majina yenu yameandikwa mbinguni. Urithi wenu ni wa hakika na wa milele."

24_edited.png

KUTUMIKIWA KWA KUWATUMIKIA WENGINE

“Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu."

27_edited.png

Anaijua Haja Yako

"Lakini Baba yetu wa mbinguni anajua kila kitu kuhusu sisi, na mahitaji yetu yote."

30_edited.png

NEEMA INAYOTAWALA

"Neema ya Mungu inashinda ukaidi wetu kwa kuumba sifa mahali ambapo haikuwepo."

100Fold Logo

NJIA ZA KUTUFUATILIA

  • Youtube
  • WhatsApp
  • Email
  • Facebook
  • Instagram
bottom of page